11/05/2021
JINSI YA KUWAFANYA WATEJA WAKUTAFUTE BADALA YA WEWE KUWATAFUTA
Kuna njia ya kisasa na bora ya kutafuta wateja ambayo k**a ukiifahamu, ukaifanyia kazi kwa kuzingatia miongozo yake utafaidika sana kupata wateja haswa kupata wateja mtandaoni.
Njia hiyo tunaiita Inbound Marketing.
Wazo kuu katika njia hii ni kuwapa walengwa wako machapisho yenye thamani kwao - yaani yenye kuwatoa sehemu fulani kuwaweka sehemu nyingine bora zaidi.
Machapisho yatakua na thamani kwa walengwa wako pale yatakapojibu kero zao, shauku zao, kuwapa miongozo na kuboresha ufahamu wao.
Unapowapa watu machapisho ya thamani unachofanya ni kuwachuja akina nani haswa unapaswa kuwasiliana nao, maana k**a sio walengwa wako, hawatoona yathamani. Pia wewe mwenyewe utajituma kufikiria yale muhimu tuu kwa aina ya watu unaowalenga.
Mfano wewe unauza samaki. mapisho la thamani kwa walengwa wako yaweza kuwa faida za samaki, jinsi ya kuwaandaa samaki, mapishi tofauti ya samaki, jinsi ya kujua k**a samaki wameharibika au la, n.k
Hivyo basi jikite kuchapisha mambo ambayo yanawagusa walengwa wako. Shida ya wajasiriamali wengi wamekua watu wa kufuata mkumbo, kupost kila kitu au kupost wanayoyapenda wao na sio yanayowalenga wateja wao watarajiwa.
Usipopost yanayowalenga wateja wako unaweza jikuta unawavuta kwako watu wengi ambao, kweli wanaweza kulike na kucomment kwenye posts zako, lakini wasije nunua bidhaa zako siku ukitangaza kwakua hao sio watu wenye 'interest' au uwezo wa kununua bidhaa zako.
Lingine la kusisitiza katika njia hii ya kupata wateja ni kuwa na subira. Unahitaji kuweka machapisho mengi, kwa muda mrefu ili ujenge kukubalika, kupendwa na kutegeemewa, kabla watu wenyewe hawajaanza kukutafuta kuuliza unauza nini au wakuulize watapataje bidhaa zako.
Hii ni njia bora sana ya kupata wateja hasa huku mtandaoni ambapo watu wamejaa wasiwasi wa kutapeliwa na kukosa imani na ubora wa bidhaa zinazouzwa.
Machapisho yako bora yatakusaidia pia kujenga brand bora ambayo itakusaidia kuwafanya watu wakuamini, na hata wewe pia uweze kuwa na bei zenye maslahi.
BOFYA LINK uendelee kujifunza mambo ya ujasiriamali kupitia WhatsApp https://chat.whatsapp.com/K3x6eo7Ri9g4TXrEPr6ed7