01/06/2026
Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF), Dkt. Tuli Salum Msuya, akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Hosteli ya Wasichana unaoendelea katika Chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) Moshi leo, tarehe 01 Juni 2026.
Mradi huo unaofadhiliwa na TaFF umefikia asilimia 35 ya utekelezaji wake na unalenga kuboresha huduma za malazi kwa wanafunzi wa k**e, kuongeza mazingira bora ya kujifunzia Chuoni hapo.
TaFF inaendelea kuwekeza katika miundombinu ya elimu ili kujenga kizazi chenye ujuzi na uwezo wa kuendeleza sekta ya misitu kwa maendeleo endelevu ya Taifa.