13/03/2026
Je,wewe ni yule mtu unayesema watanionaje watanichukuliaje au watanifikiriaje??
UNAONA AIBU
Je,wewe ni yule mtu unayesema nikishindwa je, nikifeli je, nisipofanikiwa je,au nikipoteza je??
HUWEZI KUTHUBUTU
Je,wewe ni yule mtu unayesema nitaanzaje, nitafanyaje, itakuwaje au nitawezaje??
UNAOGOPA
Leo nataka nikwambie ,hivyo vitu ndivyo vinakuletea umasikini bila wewe kujua, vinakuandaa kuwa mlalamikaji wa baadaye na vinakuandaa kuwa mtoa laana wa baadaye kwa watu wako wa karibu.
Jifunze KUTHUBUTU
Jifunze kuwa JASIRI
Jifunze KUAMINI
ukifanya hvyo vitu ,ndani ya muda utaanza kuona matokeo chanya katika Kila jambo unalolifanya.
AMUA SASA,ANZA SASA,FANYA SASA