12/11/2025
Hakuna mtu anamuumiza mwenzake kutokana na upendo au hekima. Tunaumizana kutokana na uchungu unaotokana na majeraha ya moyoni yasiyoponywa.
Wakati wowote unapohisi huzuni kutokana na kuumizwa unakuwa unaitikia uchungu wa mtu aliyekuumiza. Kila mtu ni kioo cha mwingine, means tunareflectiana. Unapoumizwa kwa maneno au matendo yangu manaake umekuwa kioo changu, kuumia kwako kunanifanya nijione kwako na wewe kwangu.
Ukweli ni huo huo pale mtu anapomtendea mwenzake mambo mema, anafanya hivyo kutokana na upendo na hekima. Katika Fizikia, hali hii huitwa transfer of energy.
Kanuni ya Umoja wa Kiungu (The Law of Divine Oneness) inasema "Kila kitu kimeunganishwa na kila kitu kingine katika uwanja mmoja mkubwa. Sisi sote ni sehemu ya mfumo mmoja wa nishati(Mungu)". “Vitu vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote.” – Yohana 1:3. Hii inamaanisha unapomtendea ubaya mtu unajiyendea mwenyewe, na upomtendea mtu wema unajitendea mwenyewe, kwasababu sisi sote asili na kiini chetu ni kimoja -Mungu; Kiswahili kina msemo "kwendako wema hurudi wema"(inamaanisha kwendako ubaya hurudi ubaya), au "wema ni akiba, hauozi". Yesu anasema "Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa".
Mathayo 7:2.
Hii pia huitwa Karma "what goes around comes around".