06/05/2026
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Mhe. Jaji George J. Kazi ( Mstari wa pili watatu kutokea kushoto), ameshiriki katika Ujumbe maalum wa Kujifunza kwa Kubadilishana Uzoefu (Peer Learning Mission) unaoendelea mjini Rome, nchini Italy kuanzia tarehe 4 hadi 8 Mei 2026,
Ujumbe huo unahusisha taasisi mbalimbali za usimamizi wa Uchaguzi kutoka jukwaa la kikanda linalojumuisha Tume za Uchaguzi kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Ukanda wa Kusini mwa bara la Afrika (Electoral Commissions Forum of SADC (ECF-SADC),
Ujumbe huo meandaliwa chini ya mfumo wa Mattei Plan, unaolenga kuwakutanisha wawakilishi kutoka nchi 18 ili kubadilishana uzoefu na taasisi za Kiitaliano zinazoshughulika na masuala ya Uchaguzi.
Mpango huo wa kimkakati wa Serikali ya Italia unalenga kusaidia Bara la Afrika katika kukuza Demokrasia.
Aidha, ujumbe huo unaungwa mkono na European Centre for Electoral Support (ECES) pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya nchini Italia.
Ushiriki wa ECF-SADC unatokana na Makubaliano ya Ushirikiano kati ya ECES na ECF-SADC yenye lengo la kuimarisha mifumo ya demokrasia ya Uchaguzi na kuboresha uendeshaji wa chaguzi huru, za haki na zenye uwazi katika ukanda huo, miongoni mwa nchi zilizopata nafasi kushiriki katika ujumbe huo ni pamoja na Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji, Lesotho, Eswatini na Zanzibar.